Monday, March 6, 2017

CHANJO ZA KUKU - RATIBA MAALUM

Image result for chanjo ya kuku    Image result for chanjo ya kuku

SIKU 1. 
 Baada ya vifaranga kutotoleshwa ndani ya siku moja wapewe glucose kwa muda wa masaa mawili. Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa na baada ya hapo vifaranga wapewe mchanganyiko wa vitamins mfano ni AMINOVIT na OTC plus


Pia hii huchanganywa na maji. Vifaranga wawekwe katika eneo lenye joto wastani na safi. Baada ya hapo siku ya pili na kuendelea vifaranga wapewe 


2.       SIKU YA 7. 
vifaranga wapatiwe chanjo ya NEWCASTLE (KIDERI). chanjo hii huchanganywa na maji safi katika eneo lenye kivuli kIsha kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili kisha toa maji hayo na kuyamwaga mbali na eneo ambalo kuku wengine wanaweza kuyafikia,au kuyachimbia.baada ya hapo vifaranga wapewe maji yenye mchanganyiko wa vitamini 


3.     SIKU YA 14. 
Wapewe chanjo ya GUMBORO(IBD). Chanjo hii pia huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga kwa muda wa masaa mawili tu, baada ya hapo vifaranga wepewe mchanganyiko wa vitamin. Kuku waliokufa kwa ugonjwa huu unaweza kuwatambua kwa kuchana vifua vyao na hapo utaona vidoti vyekundu kama hapo pichani


4.     Siku ya 21 (wiki ya tatu) 
Rudia chanjo ya Newcastle (Kideri) 


5.     SIKU 28 (Mwezi) 
Rudia chanjo ya GUMBORO IBD 


6.     SIKU 35 (Mwezi 1 na wiki 1) 
Kipindi hiki kuku wapewe mchanganyiko wa vitamin ya kutosha. 


7.     WIKI YA 6-8 
KUKU wapatiwe kinga ya Ndui (fowl pox).kinga hii sio rahisi kwa mfugaji asiye na utaalam kuwapa kuku, tafuta mtaalum wa mifugo kwa kazi hii au upate maeleze ya jinsi ya kuweka kinga hii.


8.    WIKI YA 8 

Kuku wapatiwe dawa ya minyoo kama Piperazzine na baada ya hapo unaweza kurudia chanjo ya Newcastle

Related Posts:

  • CHAKULA CHA NGURUWE NA ULISHAJI Chakula bora kwa Nguruwe ni moja  ya suala muhimu sana kwenye dhana nzima ya ufugaji wa Nguruwe wenye tija na faida kwa mfugaji. Chakula cha Nguruwe kinagharimu kama asilimia sabini ya garama zote za ufugaji wa ngur… Read More
  • DONDOO ZA ZIADA KATIKA UFUGAJI WA KUKU VITU AMBAVYO HUTAKIWI KURUHUSU KUKU WAKO WALE. Kuna baadhi ya vitu uwa tunawapa kuku kwa mazoea au tunawaachia tu tunapoona wanakula lakini ukweli vinakuwa na madhara hebu tuviangalie; VITUNGUU vitunguu… Read More
  • MAGONJWA MAKUU YA NDEGE Magonjwa huainishwa kulingana na baiolojia yao,kama Virusi,Bakteria,Kupe,ukungu,na chanzo chao,kwa mfano magonjwa ya lishe yaliyoangaliwa hapo juu.Hata hivyo,magonjwa makuu katika ndege yamegawanywa katika makundi mata… Read More
  • CHANJO ZA KUKU - RATIBA MAALUM      SIKU 1.   Baada ya vifaranga kutotoleshwa ndani ya siku moja wapewe glucose kwa muda wa masaa mawili. Glucose huchanganywa katika maji na kupewa vifaranga hawa na baada ya hapo vifaranga wap… Read More
  • MATUNZO YA WATOTO WA NGURUWE Kwa kawaida hunyonya kwa wiki 5 -8, na baada ya hapo hutengwa na mama yao na kuanza kupewa chakula chenye protini 30% kwa muda wa wiki 6 za mwanzoKUKATA MENOMara baada ya kuzaliwa watoto wakatwe meno kwa kutumia mkasi mkubwa… Read More

11 comments: